Tuesday, October 11, 2016
Vidonda vya tumbo
Ugonjwa wa vidonda vya tumbo hutokea iwapo kidonda cha ukubwa wa angalau wa nusu sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyote ya ukuta wa tumbo au utumbo wa binadamu. Kwa kawaida tatizo hili huleta maumivu makali sana ya tumbo ingawa si lazima kila maumivu ayapatayo mgonjwa husababishwa na vidonda vya tumbo.
Tafiti zimeonesha kwamba karibu asilimia 70 mpaka 90 ya vidonda vya tumbo husababishwa na aina ya vimelea vya bakteria wajulikanao kama Helicobacter pylori. Aidha matumizi ya baadhi ya dawa za kutuliza maumivu za jamii ya Non Steroid Anti-inflamatory Drugs kama Aspirin au Diclofenachuweza kusababisha au kuongeza uwezekano wa kupata ugonjwa huu.
Kuna dhana iliyozoeleka kuwa vidonda vya tumbo huathiri zaidi mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo (stomach). Dhana hii si kweli kwani sehemu inayoadhiriwa zaidi na tatizo hili ni sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo ijulikanayo kama duodenum.
💢Makundi ya PUD
Kuna makundi makuu yafuatayo ya ugonjwa huu
1. Vidonda vinavyotokea kwenye mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo(Gastric ulcers)
2. Vidonda vinavyotokea kwenye sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (Duodenal Ulcers)
3. Vidonda vinavyotokea kwenye koo(Oesophageal ulcers)
4. Vidonda vijulikanavyo kama Merckel’s Diverticulum ulcers.
💢Visababishi vya PUD
Vidonda vya tumbo husababishwa na
🔴Maambukizi ya bakteria aina yaHelicobacter pylori: Imeonekana kuwa zaidi ya asilimia 50 ya watu duniani wana vimelea hivi katika utumbo. Aidha, miongoni mwao, karibu asilimia 80 huwa hawaoneshi dalili yeyote ya kuugua ugonjwa wa vidonda vya tumbo.
Aina hii ya vimelea vya bacteria husababisha karibu asilimia 60 ya vidonda vinavyotokea kwenye tumbo (gastric ulcers) na zaidi ya asilimia 90 yaduodenal ulcers.
Hali hii husababishwa zaidi na kushindwa kwa mfumo wa kinga mwilini kuwaua na kuwaondoa kabisa vimelea hawa ndani ya mwili. Matokeo ya kushindwa huku husababisha kuwepo kwa uambukizi wa kudumu katika kuta za tumbo (chronic active gastritis), uambukizi ambao huharibu mfumo na uwezo wa kuta za tumbo kutunza homoni ya Gastrin, ambayo ni muhimu katika kuhakikisha mazingira ya tumbo yanakuwa na kiwango salama cha tindikali.
Kwa kawaida, kazi ya gastrin ni kuchochea utolewaji wa tindikali (gastric acid) kutoka kwenye seli za ukuta wa tumbo zijulikanazo kama Parietal cells.Iwapo bacteria hawa watashambulia na kuharibu ukuta wa tumbo, mfumo wagastrin pia uharibika, na hivyo kusababisha gastrin kuzalishwa kwa wingi hali ambayo pia huchochea uzalishaji wa gastric acid kwa wingi. Matokeo ya kuzalishwa kwa wingi kwa tindikali hii hupelekea kuchubuka kwa ukuta wa tumbo na hivyo kusababisha vidonda vya tumbo.
🔴Matumizi ya muda mrefu ya dawa za kuondoa maumivu za kundi la NSAIDs:Ukuta wa utumbo hujilinda na madhara yatokanayo na tindikali ya utumbo (gastric acid) kwa kuwa na utando laini (mucus) ambao hutolewa na vichocheo vijulikavyo kama Prostaglandins. Dawa hizi za kundi la NSAIDs huharibu mfumo wa kutengeza vichocheo hivi yaaniprostaglandins na hivyo kufanya kuta za tumbo kukosa utando wa kuzilinda na mashambulizi ya tindikali hali ambayo hupelekea kutokea kwa vidonda vya tumbo.
🔴Uvutaji wa sigara: Uvutaji sigara sambamba na maambukizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori huongeza madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo. Ifahamike tu kuwa uvutaji sigara pekee hausababishi vidonda vya tumbo.
🔴Vyakula au viungo vya chakula vyenye uchachu: Kinyume na dhana iliyozoeleka miongoni mwa watu wengi, baadhi ya vyakula vyenye uchachu na upilipili kama vile pilipili, ndimu, limao na masala havina uhusiano na uwezekano wa kupata vidonda vya tumbo.
🔴Watu walio katika kundi la damu la O:Imeonekana pia kwamba kundi la damu lijulikanalo kama blood group O, halina uhusiano wa kusababisha vidonda vya tumbo.
🔴Unywaji wa pombe: Unywaji wa pombe pekee hausababishi vidonda vya tumbo. Hata hivyo, unywaji wa pombe sambamba na maambukizi ya vimelea vya Helicobacter pylori huongeza madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo.
🔴Vitu vingine: Vitu vinavyohusishwa na uongezaji wa madhara ya vidonda vya tumbo ni pamoja na upasuaji wa tumbo(major abdominal surgeries), kuungua kwa moto (burns), ugonjwa wa figo; na kubadilishwa kwa viungo vya mwili kama figo au ini.
💢Dalili au viashiria vya PUD
Maumivu makali au kiungulia maeneo ya chembe moyo (epigastic pains): Maumivu juu kidogo ya tumbo mara nyingi huendana na muda wa kula chakula. Mtu mwenye vidonda kwenye tumbo (gastric ulcers) hupata maumivu makali sana kipindi anapokula au mara tu baada ya kumaliza kula wakati aliye na vidonda kwenye sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (duodenal ulcers) hupata maumivu makali anapokuwa na njaa na hupata nafuu pindi anapokula.
Kuvimbiwa au tumbo kujaa gesi. Hali hii pia yaweza kuendana na kubeua au kujamba mara kwa mara.Kucheua na kuongezeka kwa mate yanayoshuka tumboni baada ya kucheua.Kichefuchefu na kutapikaKupoteza hamu ya kula na kupungua uzitoKutapika damuKupata haja kubwa cha rangi nyeusi au kahawia chenye harufu mbaya sana. Hii humaanisha mgonjwa anapata haja kubwa au choo kilichochanganyika na damu kwa mbaliUwepo wa dalili kama kiungulia cha muda mrefu, kucheua na kutapika baada ya kula na historia ya kutumia dawa za kupunguza maumivu (NSAIDs) kwa muda muda mrefu bila kufuata ushauri wa daktari ni ishara tosha ya kumfanya mgonjwa kumuona daktari kumpima na kumfanyia uchunguzi ili kujiridhisha kuwa hana tatizo la vidonda vya tumbo.
🌟SULUHISHO KWA KUTUMIA VIRUTUBISHO VYA KIADA.🌟
🔶1) Aloe vera jel
Hichi ni kinywaji kilochotengenezwa na mmea wa aloe vera na kama inavyofahamika, aloe vera inauwezo wa kutibu vidonda tofauti ikiwemo vidonda vya tumbo. Na kila aliyetumia ameleta majibu mazuri ya kuondoa kabisa vidonda vya tumbo.
Inamanufaa mengi, manufaa mengine nimeongelea kwenye mada ya "Moyo".
🔶2) Bee Propolis
Hii imetengenezwa na nta inayotolewa na nyuki wa asali, nta hii hutumika kukinga mzinga na bacteria wanaoweza kudhuru mzinga. Lakini pia nta hii ni muhimu sana katika miili ya binadamu.
Manufaa hayo ni,
🔵ina ongeza kinga ya mwili
🔵ina saidia kuuwa bacteria hatarishi kwenye mfumo wa chakula.
🔵 Huondoa uchovu wa akili
🔵 inaongeza uwezo wa kupona
🔵 inapunguza mikonyanzi
🔵 inahusika na kutatua allergies.
Wednesday, October 5, 2016
Mwalimu wa Saikolojia....
Mmmh najua hii italeta sekeseke, ila ningependa kila mmoja atoe maoni yake. Nini msimamo wake kama ingetokea hali hii, soma story hii na andika maoni yako tu.
Siku moja katika darasa la jioni la watu wazima, mwalimu wa saikolojia aliingia darasani na kuwaambia wanafunzi;
"Nataka tucheze mchezo, mtu yeyote yule naomba ajitolee aje hapa mbele"
Mwanamke aitwae Cathy akatoka mbele. Mwalimu akamwambia aandike majina 30 ubaoni ya watu ambao anadhani ni wa muhimu katika maisha yake.
Cathy akaandika majina ya wanafamilia yake yaani mumewe na mwanae, ndugu, majirani na marafiki zake.
Mwalimu akamwambia Cathy afute majina matatu ambayo anadhani kwake sio ya muhimu sana kuzidi mengine. Cathy akafuta majina ya marafiki zake watatu.
Mwalimu akamwambia Cathy afute tena majina matano zaidi, Cathy akafuta majina ya majirani zake watano.
Hii iliendelea mpaka alipobakiwa na idadi ya watu wanne tu katika ubao. Haya yalikuwa majina ya wazazi wake, mumewe na mtoto wake wa pekee.
Darasa zima wakabaki kimya, baada ya kugundua kuwa huu sio mchezo wa Cathy peke yake sasa.
Mwalimu akamwambia Cathy afute majina mengine mawili kati ya yale manne yaliyobaki. Ulikuwa uamuzi mgumu mno kwa Cathy. Bila hiyari akafuta majina ya wazazi wake.
"Futa jingine zaidi tafadhali" mwalimu alimwambia.
Cathy akaishiwa pozi, na huku mikono ikimtetemeka na machozi katika macho yake akafuta jina la mwanae wa pekee. Na kubakiza jina la mume wake, Cathy alilia mno!!!
Mwalimu akamwambia Cathy aende akakae. Baada ya muda kidogo mwalimu akamuuliza Cathy "kwanini mume wako? Wazazi wako ndio waliokulea na kukuza, Mtoto wako ndio huyo tu mmoja uliyenae!! Na unaweza ukapata mume mwingine!!! Kwanini??"
Darasa likawa na ukimya wa hali ya juu, kila mmoja akitamani asikie ni nini Cathy atajibu.
Cathy kwa ujasiri na utulivu akainuka na kusema, "siku moja wazazi wangu watatangulia kufariki (Mwenyezi Mungu anisamehe), mtoto wangu pia ataondoka pale atakapokua mkubwa kwenda kuanzisha familia yake.
Mtu nitakayebaki nae kumaliza nae maisha hasa uzeeni ni mume wangu tu!! Yeye ndiye niliyeunganishwa nae na Mungu, mimi na yeye ni mwili mmoja."
Wanafunzi wote wakasimama na kumpigia makofi kwa kushare nao ukweli na msimamo wa maisha yake.
Huu ulikuwa uamuzi wa Cathy, yeye kwa mtizamo wake alimchagua mumewe. Je wewe ungechagua nani? Majibu yako tafadhali huku ukitaja na sababu!!
Share na wengine waje na majibu yao hapa
Asili ya Coca-cola
Asili ya Coca-Cola
Coca-Cola ni moja ya kampuni maarufu duniani, ambayo hutengenezwa soda maarufu ya Coke na vinywaji vingine vya soda. Lakini, ilikuwaje hadi ikawa na jina hilo?
Labda umewahi kusikia kwamba Coca-Cola wakati mmoja ilikuwa na kiungo cha kusisimua ambacho kiliwafanya wateja kulipenda sana. Hii ni moja ya vilivyochangia jina lake.
"Coca", kwa Kiswahili koka, ni jina la jani la mmea wa koka, moja ya viungo ambavyo mvumbuzi wa kinywaji hicho, mwanakemia wa Atlanta John Stith Pemberton, alichanganya na shira kutengeneza kinywaji chake.
Majani ya koka hutumiwa kutengeneza kokeini.
Wakati huo, mwishoni mwa karne ya 19, ilikuwa kawaida kwa majani ya koka kuchanganywa na divai na kuwa kinywaji cha kuchangamsha mwili.
Kokeini yagundulika kwenye kiwanda cha Coca-Cola
Kinywaji kipya alichotengeneza Pemberton kilikuwa njia nzuri ya kukwepa sheria zilizoharamisha uuzwaji wa pombe.
Sehemu hiyo nyingine ya jina Coca-Cola inatokana na kiungo kingine chenye nguvu, ingawa si maarufu sana.
Kiungo hiki ni kola.
Kola asili yake ni Afrika Magharibi
Ganda ambalo huwa na kokwa za kola ndani yake huwa na urefu wa inchi mbili na kabla ya kukauka, huwa za rangi ya kijani.
Ndani yake huwa na sehemu yenye fundo za rangi nyekundu au nyeupe kabla hazijakauka.
Asili ya kola ni Afrika Magharibi na zimekuwa zikitafunwa kwa miaka mingi na wenyeji kama kitu cha kuchangamsha mwili.
Kokwa hicho huwa na kafeini na theobromine, ambavyo hupatikana pia kwenye chai, kahawa na kakao. Zina pia sukari na kolanin, ambayo huaminika kuwa kichangamsha moyo.
Kufikia karne ya 19, kola zilianza kusafirishwa Ulaya na Marekani na zikaanza kutumiwa katika tembe zilizokusudiwa kutumiwa kuongeza nguvu mwilini.
Papa Leo XIII
Muda si muda, zilianza kutumiwa kwenye vinywaji. Kinywaji kimoja maarufu kilikuwa Vin Mariani, cha Ufaransa kilichotayarishwa kwa kuchanganya maji ya coca na divai nyekundu.
Kilitengenezwa na mwanakemia Mfaransa Angelo Mariani, mwaka 1863, na Papa Leo XIII alikuwa mmoja wa waliokipenda sana.
Malkia Victoria wa Uingereza, Thomas Edison, na Arthur Conan Doyle pia walikipenda sana.
Kola zilidhaminiwa sana Afrika Magharibi
Pemberton, naye alijitokeza na mchanganyiko wake akifuata mtindo huu lakini yeye hakutumia divai bali alitumia shira.
Baada ya muda kokeini iliacha kutumiwa kwenye vinywaji, baada ya kutambuliwa kama dawa ya kulevya lakini kola ziliendelea kuwa maarufu.
Kwa sasa, viungo pamoja na utaratibu wa kutayarisha soda za Coca-Cola huwa siri kuu, lakini taarifa husema huwa kola hazitumiwi tena. Badala yake, kampuni hiyo hutumia kemikali kuunda ladha sawa na ya kola.
Hata hivyo, jina halijabadilika
PICHA YA KWANZA NI MMEA WA COCA
PICHA YA PILI NI MMEA WA COLA
HAYA NDIO MAAJABU YA ZAMBIA NA MALAWI.
1. Nchi zote Malawi na Zambia zilipata uhuru mwaka 1964 na zote hutumia pesa aina ya Kwacha. Marais wake wote, Dk. Kamuzu Banda (Malawi) na Dk. Kenneth Kaunda (Zambia) walizitumikia nchi zao katika nafasi za urais kwa muda mrefu na asili zao zinatatanisha, hawaeleweki kama ni Wamalawi na Zambia. Wote Kamuzu na Kaunda walikuwa na kaulimbiu inayofanana ya “Wamuyaya” (Life) ikiwa na ishara ya mamlaka.
2. Bakili Muluzi, alizaliwa 1943, ndiye aliyechukua madaraka kutoka kwa Kamuzu Banda. Fredrick Chiluba, alizaliwa 1943, ndiye aliyechukua madaraka kutoka kwa Kenneth Kaunda, na wote wawili Muluzi na Chiluba walifanya jaribio la kutaka kubadili Katiba ili wapate kipindi cha tatu cha uongozi lakini walishindwa. Wote Muluzi na Chiluba waliwataliki wake zao kwa sababu ya kukosekana uaminifu kwenye ndoa.
3. Wote, Muluzi na Chiluba waliwapeleka watangulizi wao mahakamani (Dk. Banda na Dk. Kaunda).
4. Bakili Muluzi alimpendekeza Bingu wa Mutharika kuchukua nafasi yake, wakati Frederick Chiluba alimpendekeza Levy Mwanawasa kuchukua nafasi yake na wote waliwafanyia kampeni wakati wa uchaguzi.
5. Wote Mutharika na Mwanawasa walishinda uchaguzi na kuwa marais wa tatu katika nchi zao.
6. Muda mfupi baada ya kuchaguliwa kuwa marais, wote Mutharika na Mwanawasa walishindwa kuwabeba (kuwavumilia) watangulizi wao Muluzi na Chiluba. Wote wawili, Mutharika na Mwanawasa waliwapeleka watangulizi wao (Muluzi na Chiluba) mahakamani kwa makosa ya kujihusisha na rushwa. Sasa inavutia zaidi; Muluzi alishtakiwa na utawala wa Mutharika. Chiluba alishtakiwa na utawala wa Mwanawasa.
7. Bingu wa Mutharika alishinda kipindi cha pili cha uongozi, Mwanawasa alishinda kipindi cha pili cha uongozi. Mutharika alimchagua Joyce Banda kama Makamu wake wa Rais. Mwanawasa alimchagua Rupiah Banda kama Makamu wake wa Rais.
8. Mutharika alifariki akiwa madarakani katika kipindi chake cha pili kwa matatizo ya moyo (Cardiac Arrest). Mwanawasa pia alifariki akiwa madarakani katika kipindi chake cha pili kwa matatizo ya moyo (Cardiac Arrest).
9. Joyce Banda alichukua madaraka kutoka kwa Bingu wa Mutharika kutokana na kifo hicho. Rupiah Banda alichukua madaraka kutoka kwa Levy Mwanawasa kutokana na kifo hicho. Marais wote hawa waliochukua madaraka kutoka kwa marehemu waliitwa “Banda”!
10. Baada ya miaka 3, Rais Banda wa Zambia alishindwa kwenye uchaguzi na mpinzani wake Michael Sata. Banda wa Malawi naye ameshindwa kutetea i wake Peter
Tuesday, October 4, 2016
Maajabu ya Malawi na Zambia
HAYA NDIO MAAJABU YA ZAMBIA NA MALAWI.
1. Nchi zote Malawi na Zambia zilipata uhuru mwaka 1964 na zote hutumia pesa aina ya Kwacha. Marais wake wote, Dk. Kamuzu Banda (Malawi) na Dk. Kenneth Kaunda (Zambia) walizitumikia nchi zao katika nafasi za urais kwa muda mrefu na asili zao zinatatanisha, hawaeleweki kama ni Wamalawi na Zambia. Wote Kamuzu na Kaunda walikuwa na kaulimbiu inayofanana ya “Wamuyaya” (Life) ikiwa na ishara ya mamlaka.
2. Bakili Muluzi, alizaliwa 1943, ndiye aliyechukua madaraka kutoka kwa Kamuzu Banda. Fredrick Chiluba, alizaliwa 1943, ndiye aliyechukua madaraka kutoka kwa Kenneth Kaunda, na wote wawili Muluzi na Chiluba walifanya jaribio la kutaka kubadili Katiba ili wapate kipindi cha tatu cha uongozi lakini walishindwa. Wote Muluzi na Chiluba waliwataliki wake zao kwa sababu ya kukosekana uaminifu kwenye ndoa.
3. Wote, Muluzi na Chiluba waliwapeleka watangulizi wao mahakamani (Dk. Banda na Dk. Kaunda).
4. Bakili Muluzi alimpendekeza Bingu wa Mutharika kuchukua nafasi yake, wakati Frederick Chiluba alimpendekeza Levy Mwanawasa kuchukua nafasi yake na wote waliwafanyia kampeni wakati wa uchaguzi.
5. Wote Mutharika na Mwanawasa walishinda uchaguzi na kuwa marais wa tatu katika nchi zao.
6. Muda mfupi baada ya kuchaguliwa kuwa marais, wote Mutharika na Mwanawasa walishindwa kuwabeba (kuwavumilia) watangulizi wao Muluzi na Chiluba. Wote wawili, Mutharika na Mwanawasa waliwapeleka watangulizi wao (Muluzi na Chiluba) mahakamani kwa makosa ya kujihusisha na rushwa. Sasa inavutia zaidi; Muluzi alishtakiwa na utawala wa Mutharika. Chiluba alishtakiwa na utawala wa Mwanawasa.
7. Bingu wa Mutharika alishinda kipindi cha pili cha uongozi, Mwanawasa alishinda kipindi cha pili cha uongozi. Mutharika alimchagua Joyce Banda kama Makamu wake wa Rais. Mwanawasa alimchagua Rupiah Banda kama Makamu wake wa Rais.
8. Mutharika alifariki akiwa madarakani katika kipindi chake cha pili kwa matatizo ya moyo (Cardiac Arrest). Mwanawasa pia alifariki akiwa madarakani katika kipindi chake cha pili kwa matatizo ya moyo (Cardiac Arrest).
9. Joyce Banda alichukua madaraka kutoka kwa Bingu wa Mutharika kutokana na kifo hicho. Rupiah Banda alichukua madaraka kutoka kwa Levy Mwanawasa kutokana na kifo hicho. Marais wote hawa waliochukua madaraka kutoka kwa marehemu waliitwa “Banda”!
10. Baada ya miaka 3, Rais Banda wa Zambia alishindwa kwenye uchaguzi na mpinzani wake Michael Sata. Banda wa Malawi naye ameshindwa kutetea kiti chake na mpinzani wake Peter Mutharika.
Kwa wale wakubet ( Betting)
Watu wengi katika ulimwengu wa GAMBLING wanajikuta wakipoteza kiasi kikubwa cha pesa bila hata ya kujitambua.Ni kutokana na kutokujua au kutambua misingi kadhaa ya kushiriki katika Mchezo huu
LEO NAOMBA NIWAJULISHE WADAU WA MCHEZO JINSI AU NAMNA YA
KUSHIRIKI KIKAMILIFU NA KUFANIKIWA KUSHINDA KWA KIASI KIKUBWA.
KWA KUZINGATIA MAMBO HAYA #8 ,UTAWEZA KUFANIKIWA KUTENGENEZA FAIDA KUBWA KATIKA MCHEZO HUU.
#1 . UFANYE UWE MCHEZO,KISIWE CHANZO CHA MAPATO.
Watu wengi hufanya mchezo wa football betting kama ni kituo cha kujipatia mapato kwa ajili ya kukidhi haya mbalimbali za kimaisha kama vile
1.kulipa kodi ya nyumba,
2.Kupata ada ya watoto,
3.Kupata fedha ya kununua mali fulani i.e Pikipiki, Simu.
4. Kupata fedha ya kulipa Deni. ...na mengineyo!
Hili ni kosa kubwa sana. Unapofanya huu mchezo kama ni chanzo cha pesa kwa ajili ya suala fulani, linakupotezea nafasi ya kuweza kufanya machaguzi ya Odds
yaliyo sahihi.Watu wenye utaratibu huu ,huwa wanachagua Odds ambazo zitawaletea zao kubwa la pesa na kusahau kuwa si michezo yote katika orodha inayoweza kukupa tokeo chanya.
(Kumbuka, Mahesabu ya kina hufanywa na wenye hizi Betting Companies kuhakikisha hakuna mtu anaweza kupata kiasi kikubwa cha pesa kama matokeo ya betting(Mkeka) wake).
#2 . ZITAMBUE LIGI VIZURI.
Watu wengi hujihisisha katika huu mchezo hata bila ya kutambia mienendo (Trend) ya ligi kuu mbalimbali barani Ulaya.Kutokana na Betting Companies kuwa na aina mbali mbali za "kubet", Pia kuna baadhi ya ligi zina "facilatate successful betting" kutokana na aina ya betting.
Kwa mfano:- Ligi ya Uingereza(EPL) , inafaa sana kutumika katika kubeti katika category ya "NORMAL" kwa asilimia 80%.Hii ni kutokana na ligi kuwa na wababe wanaotabirika , Baadhi ya timu kuwa out-of-form kwa muda mrefu, Mjeruhi ya mara kwa mara.
Ligi ya Spain(LA LIGA), inafaa sana kutumika katika "NORMAL" kwa silimia 70% na "HANDCAP" kwa silimia 30%( timu za R.madrid,Barca,A.madrid)
Ligi ya Ufaransa(LIGUE 1).Kutokana na hii ligi kuto kuwa na wababe wa kueleweka , hapa ni mahali salama sana kuitumia "HANDCAP" 80% na.Pia ni ligi iliyo na idadi ndogo sana ya magoli hivyo basi "FOURTYFIVE" prediction inafaa.Hii ni kutokana na matokeo mengi ya ligi hii kuwa na tofauti ya goli moja.
Ligi kuu ya Itali (Serie A), hii ligi haina tofauti sana na ligi kuu ya Ufaransa.Baadhi ya mechi huwa na tofauti ya goli moja, na mara nyingi huwa na matokeo ya suluhu katika dakika 45 za kwanza. Hivyo "HANDCAP" ina asilimia 60% na "FOURTYFIVE" ina asilimia 40%.(Tahadhari: Hii ligi inahitaji uchambuzi wa kina katika mechi zake kabla ya kuweka bet,)
#3 . BOBEA KWENYE LIGI CHACHE TU.
Si mbaya sana ukichagua baadhi ya timu zenye nguvu kutoka ligi nyingine, bali umuhimu wa kubobea katika ligi chache ni veyma zaidi.Hii itakufanya uwe mwenye uelewa na utambuzi wa kutosha na mwenendo wa hizo ligi chache. Pia hii itakuwezesha kuweza kufanya maamuzi sahihi yaliyo na ufahamu na uelewa yakinifu.,
#4 . MARA NYINGI NI VYEMA KUFUATA HISIA.
Umeshawahi kutazama orodha ya michezo/mechi za siku husika kuanzia ya kwanza hadi ya mwisho, na katika akili yako kuna hisia/vochochezi ambavyo vina kuambia kwamba "huyu anashinda" au "huyu anafungwa" au "hii mechi suluhu"?
Basi kwa taarifa yako, hizo hisia-za-mwazo(PRESCIENCE) husadikika kuwa sahihi kwa asilimia 80%.
Hii ni kwa upande wa wale wanao-Bet katika category ya "NORMAL".
#5 . EPUKA USHABIKI.
Kuna nyakati ambazo inakuhitaji uchague mechi ambayo timu uipendayo inacheza.Hiki kimekuwa kipindi kigumu sana kwa watu wengi.Hupenda kuchagua timu zao kuwa zitashinda hata kama ukweli ni kwamba zinauwezekano mkubwa sana wa kupoteza mchezo.
Au kuwekea timu fulani ishindwe kwa mategemeo timu yake(anayoishabikia) iendelee kuongoza ligi.
Ukiona umejawa na hisia za ushabiki na huwezi shindana nazo, basi ni bora kuacha kabisa kuchagua mechi hizo.
#6 . FANYA UCHAMBUZI YAKINIFU.
Hili ni pamoja na kuzingatia aina ya mchezo unaocheza. Mfano
-NORMAL; katika hii category unashauriwa kuchagua mechi zenye timu dhaifu na imara.Hii inaleta uwezekano wa kutokea kwa matokeo yaliyo-tabiriwa.
-HANDCAP; hapa unashauriwa kuchagua mechi zenye timu ambazo zenye uwezo unaokaribia na kulingana,kwa kuwa timu moja hupewa goli la kufikirika ambayo mara nyingi huwa ni ile dhaifu basi ni vyema kuchagua matokeo ya Suluhu huku ukiamini kuwa ile timu yenye nguvu zaidi huenda ikashinda kwa tofauti isiyozidi goli 1.Yaani 2-1 au 1-0 au hata 3-2.
-FOURTYFIVE(45); hapa sasa ni mahala ambapo mechi za machaguo ya suluhu kuzingatiwa.Kutokana na mechi kuanza kwa suluhu ya bila kufungana,kuna uwezekano wa asilimia 80% ya hizo mechi kumaliza dakika 45 za kwanza bila kufungana ili uweze kuchagua suluhi ya dakika 45, inashauriwa kuchagua mechi ambazo zina upinzani mkubwa sana baina yao au mechi zenye timu zilizodhaifu sana.
#7 . JIWEKEE KIASI KATIKA KU-BET.
Huu mchezo unaathiri sana tabia-ya binadamu (Addictive).Kuna kipindi unasikia hamu ya kubet kila mara hata pale unapoona mkeka(Betting Form) umeharibika, ili tu uweze kurudisha kile kiasi cha pesa ulicholiwa.Hii hutokea kwa sababu ya kutojiwekea "kikomo".
Weka kikomo ,mfano Tsh 5000/= tu itumike ndani ya saa 72.Itakufanya uwe na kikomo katika mchezo na kukusaidia kutopoteza kiasi kikubwa cha pesa kutoka mfukoni mwako.
#8 . FUATILIA UTABIRI WA MITANDAONI.
Ni vyema kufuatilia utabili wa mitandaoni kwa sababu huwa na takwimu sinazoonyesha historia, Perfomance, na matarajio ya mechi husika.
Hakikisha una-zingatia mechi tano(5) zilizopita.
-Head-to-head ya timu hizo.
-Perfomance ya timu katika dakika 45 za kwanza
-Majeruhi walio n'je ya kikosi kikuu.
-Usajili waliofanya
-zingatia idadi ya magoli ambayo timu hizo zinafunga(score) na kufungwa(concede).
-zingatia idadi ya mechi ambazo timu imeshinda na kupoteza.
-zingatia msimamo/stance ya timu katika mechi za nyumbani na ugenini.
Kuna baadhi ya mitandao maarufu ambayo hutumika kutoa tabiri za mechi mbalimbali.
(1)windrawin.com
(2)predictZ.com
(3)soccervista.com na
(4)livescore.com tu kwa matokeo yaliyo "live" na ya mechi zilizopita.
Thursday, September 22, 2016
Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji
LEO TUANGALIE MCHANGANUO WA TSHS 300,000/= (LAKI TATU) KWA KUANZISHA MTADI WA UFUGAJI KUKU WA KIENYEJI.
Hapa tuta hitaji kuku 11 tu wakubwa wanao taga yani majike 10 na Jogoo 1 tu. Kwa kutumia kuku hao 11 baada ya miezi mitatu unaweza ukawa na kuku mia Tatu 300 au na zaidi kama unataka.
Nunua kuku wako katika chanzo cha kuaminika kuepuka magonjwa usinunue kuku sehemu za masokoni au kwenye mabanda ya njiani au kuku wanao safirishwa kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine.
Unapo nunua kuku wakubwa kwanza unapo wafikisha wape chanjo ya mdondo (Newcastle vaccine) ili kuweka rekodi yako ya chanjo maana chanjo hii hurudiwa kila baada ya miezi 3. Ukumbuke tarehe uliyo wachanja na tarehe utakayo wachanja tena baadae.
Usinunue kuku kabla hujaandaa banda na Chakula.
Katika sh. 300000 toa sh.69500 ambayo utanunua Chakula cha kuku, kuku hawa hawana formula ya Chakula hivyo unaweza kununua material ukachanganya Chakula mwenyewe ampapo utaokoa pesa nyingi pia.
Mchanganuo Wa 69500 ni:-
Pumba gunia 1. Shs.20000 gunia la pumba lina kilo 70.
- paraza kilo 25 = 700x25 =17500. Paraza ni mahindi yaliyo vunjwa vunjwa kwaajili ya Chakula cha kuku.
-mashudu ya alizeti kilo 15. 700x15=10500
- layer's consetraite
Kilo 25 kifuko. = 21500.
Ukijumlisha utakuwa umepata kilo 135 kwa shs 69500. Ambapo kila kilo moja ya Chakula utakuwa umenunua kwa shiling 514.8.
Chakula hicho kichanganye kwa kutumia chepe kichanganye vizuri kichanganyike pumba lazima iwe kavu kabisa ikaushe usiwape kuku pumba mbichi.
Kumbuka kuku anayetaga anakula Gram 130 kwa siku
Hivyo kuku 10 watakula kilo 1.3 kwa siku ambayo ni gram 1300.
Hivyo tutaweza kuona Chakula chetu kitatupeleka zaidi ya siku 100 ya zaidi ya miezi mitatu.
TOA SHS 170000 AMBAYO UTANUNULIA KUKU.
Mchanganuo wake
Kwa kila kuku mzuri ambaye ajazeeka anayetaga utampata kwa shilingi 15000 na Jogoo nzuri utampata kwa shilingi 20000.
Jogoo 1 = 20000
Majike 10 x15000= 150000 jumla 170000.
Itakuwa imebaki shs. 60500
-Hii pesa iliyobaki ni kwa ajili ya kununu material ya bei nafuu na kutengeneza banda la kuku 10 hadi 20. Kuku hawa hawaitaji banda Kubwa kwasababu hawashindi ndani wataingia ndani wakati Wa kulala jiaoni na mchana wakati wakutaga
Kuku wachiwe eneo la kutosha na lenye mchanga watakao itumia kuoga kuondoa wadudu km papasi na utitiri sehemu wanayopenda kuoga nyunyizia Dawa ya utitiri.
Banda tengeneza la kuhamisha la futi 4x8x4 yani urefu kwenda juu futi 4 upana futi 8 kipenyo futi 4. Tumia materio yaliyo karibu nawe kama mirunda, mabanzi, Mabati reject au yaliyochakaa chicken wire au wire mesh, fito mbao 2x2 au 4x2 n.k. Kama ni sehemu za mjini litakugharimu kama Tsh 50,000-60,000.Vijijini au nje ya mji ambapo miti ni mingi litakugharimu Tsh 25,000 hadi 35,000.
Haya jinsi ya kuwaendeleza hao kuku ili kupata kuku wengi hadi utakao wataka. Hapa itabidi ukubali kupeleka Mayai sehemu ambapo wanatotolesha ambapo trey 1 ni shilingi 10000.
Hapa kuku hawa 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku ambapo kwa mwezi ni Mayai 240. Kila baada ya siku 7 peleka Mayai kwenye Mashine yakutotolea (incubator). Hivyo kwa mwezi utapeleka Mayai 240 utapata wastani Wa Vifaranga 200. Hivyo baada ya mwezi nakushauri usitotoleshe tena hao Vifaranga 200 ni wengi sana kwa kuanzia kwa kuwa tayari tunenunua Chakula cha kuku cha kutupeleka miezi mitatu basi Mayai utakayo endelea kuokota utayauza kwaajili ya kupata hela ya Chakula cha Vifaranga watakao toka hao zaidi ya 200. Hivyo mradi huu utakuwa unajiendesha wenyewe. Nikiwa na maana kama kuku 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku na Mayai 240 kwa mwezi ni wazi kwamba kuku hao wanakuingizia 120000 kwa mwezi ambaya sasa hela Hii itatumika kununua Chakula cha kulea hao Vifaranga ambapo Mayai ya mwezi tu yataweza kununua Chakula ambacho Vifaranga 200 watakula mwezi pamoja na chanjo na Dawa zote.
Hivyo baada ya miezi mitatu utakuwa na Vifaranga wakubwa Wa miezi miwili na Chakula cha kuku wakubwa ndo kitakuwa kinaishia hapa utachanganya Chakula cha aina moja tu wale Vifaranga watakuwa wameshakuwa kiasi cha kula Chakula chochote.
Wednesday, September 21, 2016
TUJIFUNZE KUPITIA HILI
USIPITE BILA KUSOMA HII
Siku moja jioni katika mji flani, kulikuwa na basi likisafiri kutoka mji huo kuelekea mji mwingine. Lilikuwa ni basi kubwa na limejaa abiria. Wakati wakiendelea na safari, ghafla, mvua kubwa iliyoambatana na radi ikaanza kunyesha. Dereva hakuogopa, wala abiria, wakaendelea na safari. Mara wakati wanaenda, radi ikaanza kufuatilia gari. Kila wakienda, radi inapiga karibu na basi kana kwamba inalifuata basi. Likisimama, radi inapiga pembezoni mwa basi. Dereva kuona hivyo, akasimamisha gari mita 5 kutoka kwenye mti... Akawaambia abiria, "Humu ndani ya basi, kuna mtu ambaye leo ni siku yake ya kufa, tena kufa kwa radi. Ili tusife wote, nataka kila abiria ashuke akaguse mti ili anayepigwa na radi, apigwe wengine wasife kwa ajili yake. "Abiria wakitetemeka, wakaanza kushuka mmoja mmoja. Unaenda unagusa mti , kisha unarudi kwenye basi. Abiria wote pamoja na dereva mmoja mmoja, wakaenda, wakagusa mti na kurudi bila dhara lolote! Akawa kabaki abiria mmoja tu, ambaye alikuwa hajagusa mti. Abiria wote kwa macho ya hasira wakamwambia akaguse mti. Akawa anaogopa kufa. Akagoma. Wakamlazimisha kwa nguvu sana na kumtoa nje....... ........ Yule abiria akiwa amefumba macho, akaenda akagusa mti. Hamadi bin Vuu! Radi kali sana ikalipiga basi, abiria na wote waliokuwamo, wakafa palepale. Kumbe uwepo wake ndio ulikuwa unazuia abiria wengine wasidhurike na radi.
MAFUNZO
1. Unapofanikiwa, huwezi jua uwepo wa nani umefanikisha mafanikio yako, usichukue sifa zote peke yako. Wapatie na wengine bila kumsahau MUNGU.
2. Unaweza kujiona huna thamani sehemu ulipo, iwe kwenye kundi la WhatsApp, darasani, kazini, kwenye basi, barabarani bila kujua kama uwepo wako ni wa muhimu sana kwa ustawi wa wengine.
3. Usimtenge wala kumnyanyasa mtu au jirani yako, huwezi jua uwepo wake ni kwa ajili gani.
Comment neno 'ASANTE MUNGU' kwa ulinzi anaotupa na mema anayotutendea kila siku kisha SHARE na wengine
Tuesday, September 20, 2016
Adobe photoshop
Somo la leo
Tutaona maana ya tools tofauti za Photoshop
Move tool ina fanya kazi ya move picha
Marquee tool ina fanya kazi yaku select kwenye kazi iufanyayo.
polygonal tool nayo inafanya kazi kama marquee tool ila apa ina kuwa tofauti kidogo maana una select sehemu utakayo wewe, tofauti na marquee
Kwenye polygonal tool
Kuna
lasso tool
Polygonal lasso too
magnetic lasso tool
Izo tool zina utofauti ila kazi yake ni moja tu ambaoyo ni ku select
Crop tool uyu jamaa yeye anafanya kazi ya kuongeza nafasi ya gazi yako unayo ifanya. Kwamfano, ulifungua seemu ndogo kama
Width 500 pixels
Height 500 pixels
Resolution 300 pixel/inch
Na ukiona kuwa kazi yako nikuwa na seemu yakuifanyia iyo kazi ni ndogo unaweza kuongeza au kupunguza pia.
eyedropper tool ina fanya kazi ya kuchagua rangu kwenye kazi unayo ifanya kwamfano
Ukiwa una chora cartooneyes
Kwajili yakupata rangi uitakayo kiuraisi eyedropper tool
Ina saidia kwa ilo.
patch tool
Uyu jamaa anafanya kazi sana kwa wa manipulator
Inafanya kazi ya ku select sehemu fulani na kuiweka kwenye seemu nyingine,
Kama, uki select seemu la jicho alafu ukichukuwa seemu iyo nakuipeleka seemu nyingine kama mdomo, kwenye seemu ya jicho kutachukuwa seemu ile ya mdogo.
Iyo ni mfano tu.
Spot Healing brush
Inafanya kazi ya kufuta kama mfano wa watu wenye chunusi, madoa doa kwemye mwili wao iyo apo inasaidia sana kuondoa uchafu uo.
Brush too iyo inafanya kazi ya kupaka rangi na kwa wachoraji ila sio tu kupaka rangi, ila kazi yake kubwa ni iyo.
Eraser tool uyu jamaa yeye uwa ni muaribifu wa ali ya juu, yani kazi yake yeye ni kufuta tu.
Ila kwenye iyi kuna eraser tofauti kama,
Background eraser tool
Yeye anafanya kazi kufuta vitu vilivyo nyuma ya photo, sio kama aifuti mbele ya photo ila inapashwa uwe makini na ukifanyacho.
Magic eraser tool uyu mi nampendaga sana yeye anakuaga mwerevu sana na uko fasa sana kwaku futa utakacho,
Ila kuwa makini sana na magic eraser tool kwenye picha ambayo ina rangi nyingi maana uyu jamaa akikutana tu na picha kama iyo yeye alikini uwa anachanganikiwa sana,
Yeye anafanya kazi zaidi kwenye picha ya rangi moja au rangi mbili au tatu.
Gradient tool wenye kujuwa kuandika uwa wana mtumia sana uyu jamaa kwa kuwapa manjonjo ya rangi nzuri wazitakazo. Kama rangi za zahabu/ gold na kazalika, ata wachoraji cartoon wengine wana mtumia pia.
Paint brucket tool
Iyi apa nikama beseni la rangi, lina saidia kubadili rangi pia, kwamfano uki select then una mtupia uyu jamaa selection yako inakuwa imepakwa rangi tayari.
Pen toolyeye anafanya kaza ya ku select seemu pia.
Uyu jamaa anafanya kazi sana kwenye kazi nyingi.
Apa tuko na
horizontal type tool apa ni kwandika tu.
kuna
Zoom kwajili yaku zoom picha yako au nafasi ya kazi yako.
Asannte wengine wata malizia apo naona ndio vitu muimu kujuwa apo
Monday, September 19, 2016
NANI KAMA MAMA
KISA CHA KUSISIMUA
Kuna kijana mmoja daktari alikwenda kuposa. Binti aliyemposa akamuwekea masharti mazito. Akamwambia chagua mawili imma kunioa mimi au kukaa na mama yako, kwa sababu ukinioa mimi sitokubali mama yako aje hata harusini kwangu! Yule kijana aliemewa. Hakujua la kufanya. Mke anamtaka, lakini mama yake pia anampenda. Hivyo aliamua kuomba ushauri kwa mwalimu wake wa chuo kikuu. Alimwambia: moyo wangu unampenda mno binti niliyekwenda kumposa, lakini pia siwezi kuishi mbali na mama yangu. Nifanye nini?
Yule mwalimu mwenye hekima ambaye alikuwa anajua tabu alizopitia mama wa kijana yule, alimjibu kwa kumwambia: Kabla ya kukueleza uchague yupi kati ya wawili hao, rudi nyumbani, na leo usifanye chochote, ila kuikosha mikono ya mama yako. Yule kijana alifanya kama alivyotakiwa na mwalimu wake. Alipofika nyumbani aliomba idhini kwa mama yake amruhusu kuikosha mikono yake, na yule mama alimkubalia bila ya ajizi yoyote. Yule kijana alipoanza kuikosha mikono ya mama yake na kuona jinsi ilivyogugutaa kwa kazi za sulubu, alilia sana. Muda wote huu alikuwa hajawahi kuangalia viganja vya mama yake. *Je, na wewe umewahi kukaa na kuangalia viganja vya mama au baba yako kuona tabu walizopitia kukulea?* Kumbe baba wa yule kijana alifariki dunia yeye akiwa bado mdogo, yule mama aliamua kusamehe kila kitu kwa ajili ya mustakbali wa mwanawe. Alijitolea kufanya kazi za sulubu. Alikubali kuwa mtumishi wa ndani, kukosha nguo, kupiga deki na kila kazi ambayo alihisi ingelimletea chumo la halali bila ya kujali ugumu wa jkazu hiyo. Juhudi zake zilizaa matunda na kufanikiwa kumlea na kumsomesha mwanawe hadi chuo kikuu na sasa ni daktari ambaye ana mustakbali mzuri. Baada ya yule kijana kukumbuka yote hayo, alifanya haraka kumpigia simu mwalimu wake huku macho yakiendelea kububujikwa na machozi akimwambia, siwezi kusubiri hadi kesho. Jibu nimeshalipata. Siwezi kumtupa mama yangu kwa ajili ya mtu asiyejua thamani ya mama. Ahsante sana kwa kunionesha njia sahihi! Kamwe siwezi kumuuza mama yangu kwa ajili ya leo yangu wakati yeye ameuza maisha yake yote kwa ajili ya mustakbali wangu.
NANI KAMA MAMA?!? Maa! Tabasamu lako ni ufunguo wangu wa ofanisi.
Kama umeipenda.
Share kwa wengine ili nao wazinduke.
Ni muda upi sahihi kuingia kwenye mahusiano
Ninarudia tena (Zingatia hii ni Muhimu )
SOMO : NI MUDA UPI NI SAHIHI KWA MTU KUINGIA KWENYE MAHUSIANO MAPYA BAADA YA MAHUSIANO YALE YA KWANZA KUVUNJIKA.
●Watu wengi wanakurupuka na matokeo yake wanajikuta kila kukicha wanaumizwa kiasi kwamba hawana tena hamu na mahusiano tena, wamekata tamàa, hawaamini kama kuna mtu mwaminifu, hawataki kusikia habari za mahusiano, zaidi ya Yote hata kuna wengine walifanya maamuzi ya kuoa /kuolewa si kwa sababu wanapenda ila kwa sababu ni umri tu umewatupa mkono hivyo wakaamua kudumbukia popote ila upendo hakuna, japo wameolewa ila moyoni hampendi aliye naye kwa 100%.Kwa hiyo yupo 50/50.
■NI MUDA GANI HASA UNATAKIWA KUINGIA KWENYE MAHUSIANO MAPYA
1.Ni Muda ambao una uhakika kuwa ,UKIMUWAZA EX ALIYE KUUMIZA, NDANI YAKO HAUPATI UCHUNGU.
2.Ni Muda ambao Umekwisha kutafakari kwa kina na kupata majibu juu ya sababu zilizokufanya ulie kwenye uhusiano uliokuliza na Ex wako. Maàndiko yanasema siku ya mabaya utafakari. Tafakari usije ukarudia kosa lile lile.
3.Ni Muda ambao Moyoni Mwako hauoni kama kuna sababu ya kurudiana na Ex wako.Kama unaona bado unampenda usitafute mtu mwingine maana utamsumbua kwa sababu moyo wako hautakuwa kwake bali kwa ex wako.
4.Ni Muda ambao Moyoni Mwako umemsamehe yule aliye kujeruhi na upo Tayari kumuacha aendelee na maisha yake pasipo kinyongo.
5.Ni Muda ambao mawazo yako hayapo Tayari kufanya maamuzi ya kutafuta mtu mwingine kwa nia ya kumkomoa ex wako, yaani kutaka kumkomeshea. Maana hapo ni kujiumiza mwenyewe na hayo ni maisha yako si ya ex wako.
6.Ni Muda ambao UMEMUOMBA MUNGU VYA KUTOSHA HADI MOYONI MWAKO UNAYO AMANI YA KRISTO
7.Ni Muda ambao UHUSIANO WAKO NA MUNGU HATA WEWE UKIJIKAGUA UNAONA KABISA UPO VIZURI SANA. Unajua Watu wengi mahusiano yao na wapenzi wao huwa yakivurugika hata mahusiano yao na MUNGU yanaharibika SANA.
8.Ni Muda ambao ukisikia habari za Ex wako haukasiriki na unaona hayo ndiyo maisha yake aliyoyachagua.
9.Ni Muda ambao umerelax na unautumia Muda wako mwingi kumtumikia MUNGU kwenye kusudi alilokuitia.
NB: VIGEZO HIVYO HAPO JUU NI DALILI NZURI KUWA SASA UPO TAYARI. UKIONA KUNA SEHEMU UNAKWAMA MUOMBE MUNGU AKUSAIDIE, NAYE ATAKUSAIDIA.
MUNGU AKUBARIKI
SOMO : NI MUDA UPI NI SAHIHI KWA MTU KUINGIA KWENYE MAHUSIANO MAPYA BAADA YA MAHUSIANO YALE YA KWANZA KUVUNJIKA.
●Watu wengi wanakurupuka na matokeo yake wanajikuta kila kukicha wanaumizwa kiasi kwamba hawana tena hamu na mahusiano tena, wamekata tamàa, hawaamini kama kuna mtu mwaminifu, hawataki kusikia habari za mahusiano, zaidi ya Yote hata kuna wengine walifanya maamuzi ya kuoa /kuolewa si kwa sababu wanapenda ila kwa sababu ni umri tu umewatupa mkono hivyo wakaamua kudumbukia popote ila upendo hakuna, japo wameolewa ila moyoni hampendi aliye naye kwa 100%.Kwa hiyo yupo 50/50.
■NI MUDA GANI HASA UNATAKIWA KUINGIA KWENYE MAHUSIANO MAPYA
1.Ni Muda ambao una uhakika kuwa ,UKIMUWAZA EX ALIYE KUUMIZA, NDANI YAKO HAUPATI UCHUNGU.
2.Ni Muda ambao Umekwisha kutafakari kwa kina na kupata majibu juu ya sababu zilizokufanya ulie kwenye uhusiano uliokuliza na Ex wako. Maàndiko yanasema siku ya mabaya utafakari. Tafakari usije ukarudia kosa lile lile.
3.Ni Muda ambao Moyoni Mwako hauoni kama kuna sababu ya kurudiana na Ex wako.Kama unaona bado unampenda usitafute mtu mwingine maana utamsumbua kwa sababu moyo wako hautakuwa kwake bali kwa ex wako.
4.Ni Muda ambao Moyoni Mwako umemsamehe yule aliye kujeruhi na upo Tayari kumuacha aendelee na maisha yake pasipo kinyongo.
5.Ni Muda ambao mawazo yako hayapo Tayari kufanya maamuzi ya kutafuta mtu mwingine kwa nia ya kumkomoa ex wako, yaani kutaka kumkomeshea. Maana hapo ni kujiumiza mwenyewe na hayo ni maisha yako si ya ex wako.
6.Ni Muda ambao UMEMUOMBA MUNGU VYA KUTOSHA HADI MOYONI MWAKO UNAYO AMANI YA KRISTO
7.Ni Muda ambao UHUSIANO WAKO NA MUNGU HATA WEWE UKIJIKAGUA UNAONA KABISA UPO VIZURI SANA. Unajua Watu wengi mahusiano yao na wapenzi wao huwa yakivurugika hata mahusiano yao na MUNGU yanaharibika SANA.
8.Ni Muda ambao ukisikia habari za Ex wako haukasiriki na unaona hayo ndiyo maisha yake aliyoyachagua.
9.Ni Muda ambao umerelax na unautumia Muda wako mwingi kumtumikia MUNGU kwenye kusudi alilokuitia.
NB: VIGEZO HIVYO HAPO JUU NI DALILI NZURI KUWA SASA UPO TAYARI. UKIONA KUNA SEHEMU UNAKWAMA MUOMBE MUNGU AKUSAIDIE, NAYE ATAKUSAIDIA.
MUNGU AKUBARIKI
Thursday, September 15, 2016
Magonjwa Ya Figo
*SABABU ZA MAGOJWA YA FIGO. JIHADHARI NA ONYEKA!.*
Raia wa Ghana wanazidi kufa kwa matokeo ya ugonjwa wa Figo.
*JINSI YA KUONDOKANA NA JANGA HATARI LA UGONJWA WA FIGO:*
*1.Usichelewe kwenda HAJA.* Kutunza mkojo kweye kibofu chako kwa muda mrefu ni wazo baya. Kibofu kikijaa kinaweza kusababisha uharibifu. Mkojo ambao unakaa kwenye kibofu huzidisha bakteria haraka.
Mara mkojo unaporudi nyuma ya njia na Figo, sumu dutu husababisha maambukizi ya figo, pia njia ya mkojo na "nephritis", pamoja na "uremia". Wakati wito asili (unahisi mkojo) fanya hivyo haraka iwezekanavyo.
*2. Kula Chumvi kupita kiasi.* Inatupasa kula Chumvi isiyozidi 5.8 gramu kwa siku.
*3. Kula nyama kupita kiasi.*
Protini ikizidi sana katika mlo wako inadhuru figo zako. Mmeng'enyo wa Protini unazalisha amonia- sumu dutu ambayo ina uharibifu mkubwa kwa figo zako. Nyama nyingi inaleta uharibifu zaidi wa figo.
4. *Unywaji mwingi wa "Caffeins".*
Caffein hutokana na vinywaji vya Soda na vinywaji vingine laini kama Kahawa, Redblue n.k. Hupandisha shinikizo la damu na figo zako kuanza mateso. Unapaswa kupunguza kiwango cha Coke, Pepsi, Red Bull, nk ambavyo hunywa kila siku.
*5. Kutokunywa maji.*
Figo zetu lazima zichakatwe vizuri kutekeleza majukumu yake vizuri. Endapo hatunywi ya kutosha, sumu dutu inaweza kuanza kukusanyika katika damu, kama hakuna kimiminika cha kutosha kutoa kwa njia ya figo. *** Kunywa zaidi ya bilauri 10 za maji kila siku.
Kuna njia rahisi ya kuangalia kama unakunywa maji ya kutosha: Angalia rangi ya mkojo wako; Wepesi wa rangi, ndiyo vzuri.
*6. Kuchelewa matibabu.*
Tibu matatizo yako yote ya kiafya kwa uhakika na uwe unachunguza afya yako mara kwa mara. Wapendwa na wapenzi wangu, hebu tujisaidie wenyewe... Shirikisha wengine, kama unajali. ----------------
*Pia epuka vidonge hivi, ni hatari sana:*
D- baridi*
Vicks Action- 500*
Actified*
Coldarin*
Cosome*
Nice*
Nimulid*
Cetrizet- D
Hivi vidonge vina Phenyl propanol- amide PPA ambayo husababisha stroke na ni marufuku Marekani.
MWISHO... Tafadhali, kabla ya kufuta, msaidie rafiki yako kwa kumpitishia hii..!
*Inaweza kumsaidia mtu!*
Wasambazie wengi kwa kadiri uwezavyo.
Shirikisha ujumbe huu kwa mpendwa wako.
*Maonyo muhimu ya Afya*
1. Jibu (pokea) simu wito na sikio la kushoto.
2. Usinywe dawa zako kwa maji baridi....
3. Usile milo mizito baada ya saa 11 jioni.
4. Kunywa maji vuguvugu mengi asubuhi na kiasi usiku. Usinywe maji baridi kamwe.
5. Muda bora wa kulala ni kutoka saa 4 usiku hadi saa 10 Alfajiri.
6. Usilale mapema baada ya kumeza dawa au baada ya mlo. Usiku, Kula chakula laini.
7. Usipokee simu yako ikiwa haina chaji. Wakati huo mionzi huwa ina nguvu mara 1000 .
Je, unaweza kuwasambazia watu unao wajali?
Mimi nimeshafanya kwenu....!!.
Raia wa Ghana wanazidi kufa kwa matokeo ya ugonjwa wa Figo.
*JINSI YA KUONDOKANA NA JANGA HATARI LA UGONJWA WA FIGO:*
*1.Usichelewe kwenda HAJA.* Kutunza mkojo kweye kibofu chako kwa muda mrefu ni wazo baya. Kibofu kikijaa kinaweza kusababisha uharibifu. Mkojo ambao unakaa kwenye kibofu huzidisha bakteria haraka.
Mara mkojo unaporudi nyuma ya njia na Figo, sumu dutu husababisha maambukizi ya figo, pia njia ya mkojo na "nephritis", pamoja na "uremia". Wakati wito asili (unahisi mkojo) fanya hivyo haraka iwezekanavyo.
*2. Kula Chumvi kupita kiasi.* Inatupasa kula Chumvi isiyozidi 5.8 gramu kwa siku.
*3. Kula nyama kupita kiasi.*
Protini ikizidi sana katika mlo wako inadhuru figo zako. Mmeng'enyo wa Protini unazalisha amonia- sumu dutu ambayo ina uharibifu mkubwa kwa figo zako. Nyama nyingi inaleta uharibifu zaidi wa figo.
4. *Unywaji mwingi wa "Caffeins".*
Caffein hutokana na vinywaji vya Soda na vinywaji vingine laini kama Kahawa, Redblue n.k. Hupandisha shinikizo la damu na figo zako kuanza mateso. Unapaswa kupunguza kiwango cha Coke, Pepsi, Red Bull, nk ambavyo hunywa kila siku.
*5. Kutokunywa maji.*
Figo zetu lazima zichakatwe vizuri kutekeleza majukumu yake vizuri. Endapo hatunywi ya kutosha, sumu dutu inaweza kuanza kukusanyika katika damu, kama hakuna kimiminika cha kutosha kutoa kwa njia ya figo. *** Kunywa zaidi ya bilauri 10 za maji kila siku.
Kuna njia rahisi ya kuangalia kama unakunywa maji ya kutosha: Angalia rangi ya mkojo wako; Wepesi wa rangi, ndiyo vzuri.
*6. Kuchelewa matibabu.*
Tibu matatizo yako yote ya kiafya kwa uhakika na uwe unachunguza afya yako mara kwa mara. Wapendwa na wapenzi wangu, hebu tujisaidie wenyewe... Shirikisha wengine, kama unajali. ----------------
*Pia epuka vidonge hivi, ni hatari sana:*
D- baridi*
Vicks Action- 500*
Actified*
Coldarin*
Cosome*
Nice*
Nimulid*
Cetrizet- D
Hivi vidonge vina Phenyl propanol- amide PPA ambayo husababisha stroke na ni marufuku Marekani.
MWISHO... Tafadhali, kabla ya kufuta, msaidie rafiki yako kwa kumpitishia hii..!
*Inaweza kumsaidia mtu!*
Wasambazie wengi kwa kadiri uwezavyo.
Shirikisha ujumbe huu kwa mpendwa wako.
*Maonyo muhimu ya Afya*
1. Jibu (pokea) simu wito na sikio la kushoto.
2. Usinywe dawa zako kwa maji baridi....
3. Usile milo mizito baada ya saa 11 jioni.
4. Kunywa maji vuguvugu mengi asubuhi na kiasi usiku. Usinywe maji baridi kamwe.
5. Muda bora wa kulala ni kutoka saa 4 usiku hadi saa 10 Alfajiri.
6. Usilale mapema baada ya kumeza dawa au baada ya mlo. Usiku, Kula chakula laini.
7. Usipokee simu yako ikiwa haina chaji. Wakati huo mionzi huwa ina nguvu mara 1000 .
Je, unaweza kuwasambazia watu unao wajali?
Mimi nimeshafanya kwenu....!!.
Samatta katika EUROPA
Leo Mbwana Samatta na klabu yake ya FC Genk ya Ubelgiji
watakuwa ugenini kukipiga dhidi ya Rapid Wien ya Australia kwenye Ligi ya EUROPA.
Neno moja la kumtakia heri Samatta kwenye mchezo huo
watakuwa ugenini kukipiga dhidi ya Rapid Wien ya Australia kwenye Ligi ya EUROPA.
Neno moja la kumtakia heri Samatta kwenye mchezo huo
Ronaldo na rekodi zake
Mtaalamuu kaweka na kuvunja rekodi UEFA
goal alilofunga mtalamu cr7 kwa njia ya FAULO JANA LIMEMFANYA AFIKISHE FAULO 12 KATIKA MICHUANO HYO NA KUVUNJA RECODI YA DEL PIERO MWENYE MAGOLI 11
mm namwitaa MZEE wa marekodi
goal alilofunga mtalamu cr7 kwa njia ya FAULO JANA LIMEMFANYA AFIKISHE FAULO 12 KATIKA MICHUANO HYO NA KUVUNJA RECODI YA DEL PIERO MWENYE MAGOLI 11
mm namwitaa MZEE wa marekodi
Wednesday, September 14, 2016
UTAPIAMLO KWA WATOTO UNAEPUKIKA!!!!
UTAPIAMLO KWA WATOTO UNAEPUKIKA!
Je, wajua kwamba kwa takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) asilimia 45 ya vifo vya watoto chini ya miaka mitano vinatokana na lishe duni?
Je, wajua kwamba watoto wa kundi hili wapatao milioni tano na laki 9 walifariki duniani mwaka 2015 pekee?
OKOA MAISHA YA MWANAO KWA KUMPATIA MLO KAMILI ULIOSHAMIRISHWA NA VIINI LISHE
Je, wajua kwamba kwa takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) asilimia 45 ya vifo vya watoto chini ya miaka mitano vinatokana na lishe duni?
Je, wajua kwamba watoto wa kundi hili wapatao milioni tano na laki 9 walifariki duniani mwaka 2015 pekee?
OKOA MAISHA YA MWANAO KWA KUMPATIA MLO KAMILI ULIOSHAMIRISHWA NA VIINI LISHE
SEMI MBALIMBALI TUNAZOZIISHI KATIKA JAMII
NI USEMI UPI UMEKUKAMATA?:
1. "Kuzaliwa masikini siyo kosa lako,ila kufa masikini ni ujinga wako." ~ Bill Gate
2. "Kushindwa kupanga ni kupanga kushindwa." ~ Felix Bundala
3. "Heri kufa na mawazo yanayoishi, kuliko kuishi na Mawazo yaliyokufa." ~ Che Guevara
4. "Vita inamalizwa kwa vita na ili tuachane na matumizi ya bunduki inabidi itumike bunduki." ~ Mao ze Dong
5. "Sitamani kumjua babu yangu alikuwa nani, ninachotaka kumfahamu mjukuu wake atakuwa na tabia gani." ~ Martin Luther King
6. "Usimuulize mtu yoyote anayenijua mimi maana utamjua yeye kupitia mimi." Joe Lescot
7. "Muonekano siku zote hutengeneza uwezekano." ~ Lucky Crackent
8. "Hatuwapendi wanawake kwa sababu ni wazuri, ila tunawaona wazuri kwa sababu tunawapenda." ~ Luck Crackent
9. "Watu ni wengi ila binadamu ni wachache." ~ Fidel Castro
10. "Usiishi kwa sababu unaishi, tafuta sababu ya wewe kuishi." ~ Jay Ozil Cazorla Wilshere
11. "Hakuna mkate mgumu mbele ya chai." ~ Bob Sydou
12. "Kichwa kikubwa bila Akili ni Adhabu kwa miguu." ~ Thabiti Kube..
1. "Kuzaliwa masikini siyo kosa lako,ila kufa masikini ni ujinga wako." ~ Bill Gate
2. "Kushindwa kupanga ni kupanga kushindwa." ~ Felix Bundala
3. "Heri kufa na mawazo yanayoishi, kuliko kuishi na Mawazo yaliyokufa." ~ Che Guevara
4. "Vita inamalizwa kwa vita na ili tuachane na matumizi ya bunduki inabidi itumike bunduki." ~ Mao ze Dong
5. "Sitamani kumjua babu yangu alikuwa nani, ninachotaka kumfahamu mjukuu wake atakuwa na tabia gani." ~ Martin Luther King
6. "Usimuulize mtu yoyote anayenijua mimi maana utamjua yeye kupitia mimi." Joe Lescot
7. "Muonekano siku zote hutengeneza uwezekano." ~ Lucky Crackent
8. "Hatuwapendi wanawake kwa sababu ni wazuri, ila tunawaona wazuri kwa sababu tunawapenda." ~ Luck Crackent
9. "Watu ni wengi ila binadamu ni wachache." ~ Fidel Castro
10. "Usiishi kwa sababu unaishi, tafuta sababu ya wewe kuishi." ~ Jay Ozil Cazorla Wilshere
11. "Hakuna mkate mgumu mbele ya chai." ~ Bob Sydou
12. "Kichwa kikubwa bila Akili ni Adhabu kwa miguu." ~ Thabiti Kube..
Lionel Andres Messi
HIV NDIVYO ILIVYO , MGUU 1 WA MESI N ZAID YA MIGUU 22 YA WACHEZAJ WA CELTC : Lig ya mabngwa baran Ulaya ilianza rasmi hapo jana kwa michezo 7 ya makundi A-D huku mechi zngine 9 zkipgwa leo kuanzia kundi E-H , pa1 na mchezo wa kiporo wa kundi C kat ya Ct v/s Borusia moncheng gladbach . Ktk mchezo pekee wa kundi C kat ya FC BARCA v/s CELTC mvua ya magol iliwashukia Celtc ikiôngozwa na Brendan Rodgers Pa1 na baadh ya majna toka EPL kama , Kolo-2re , Adam Amstong , Sinclair na Boyata , huku mesi akifunga hat trick ktk mchezo huo . Mbali na hat trick Mesi amewaongoza wachezaj kutoka AMERIKA KUCN toka nchi 4 za ARGENTNA , BRAZIL , URUGUAY na CHILE kufunga gol 11 kat ya 22 yaliofungwa jana , huku mengine 11 yakiongozwa na mjeruman Joshua Kimmich kufungwa na wachezaj wa Ulaya toka mataifa 4 tofaut ambayo n SPAIN , POLAND , SWITSLAND na GERMANY . Sasa swali je , Cr7 ata wakomboa Celtc leo?
Mwenyekiti wa bunge aomba radhi
Mwenyekiti wa Bunge amwomba radhi Mbowe
Hatua hiyo imefutia mwongozo ulioombwa na wabunge wawili Chadema, kuwa mchango wa Mbowe haukutambulika licha ya kufika Bukoba, kutoa misaada na kushirikiana na waathirika wa tukio hilo hadi sasa.
Aliyeanza kuomba mwongozo ni Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche ambaye alihoji kwa nini mwenyekiti huyo wa Bunge amewatambua viongozi waliofika eneo la tukio na kutoa misaada lakini ameshindwa kumtambua Mbowe ambaye mpaka sasa yupo eneo la tukio na ametoa msaada.
Mbunge mwingine ni Pascal Haonga wa Mbozi ambaye alisema Mbowe ni kiongozi mkubwa na halitakuwa jambo la maana kama mchango wake hautatambulika kwani suala hilo siyo la kisiasa.
Kufuatia mwongozo huo, Zungu aliomba radhi na kuongeza kuwa anamtambua Mbowe kama kiongozi aliyetoa msaada kwa waathirika hao.
Awali, Mwenyekiti huyo wa Bunge baada ya kuingia ukumbini alitoa pole kwa waathirika wa tetemeko hilo lililoua watu 17 na kuwatambua watu waliochangia tukio hilo akiwamo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na wafanyabiashara.
Baada ya kipindi cha maswali na majibu kuisha, mwenyekiti huyo aliwatambua wafanyabiashara wengine waliotoa msaada kwa waathirika hao lakini hakugusia msaada ulitolewa na Mbowe.
Hatua hiyo imefutia mwongozo ulioombwa na wabunge wawili Chadema, kuwa mchango wa Mbowe haukutambulika licha ya kufika Bukoba, kutoa misaada na kushirikiana na waathirika wa tukio hilo hadi sasa.
Aliyeanza kuomba mwongozo ni Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche ambaye alihoji kwa nini mwenyekiti huyo wa Bunge amewatambua viongozi waliofika eneo la tukio na kutoa misaada lakini ameshindwa kumtambua Mbowe ambaye mpaka sasa yupo eneo la tukio na ametoa msaada.
Mbunge mwingine ni Pascal Haonga wa Mbozi ambaye alisema Mbowe ni kiongozi mkubwa na halitakuwa jambo la maana kama mchango wake hautatambulika kwani suala hilo siyo la kisiasa.
Kufuatia mwongozo huo, Zungu aliomba radhi na kuongeza kuwa anamtambua Mbowe kama kiongozi aliyetoa msaada kwa waathirika hao.
Awali, Mwenyekiti huyo wa Bunge baada ya kuingia ukumbini alitoa pole kwa waathirika wa tetemeko hilo lililoua watu 17 na kuwatambua watu waliochangia tukio hilo akiwamo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na wafanyabiashara.
Baada ya kipindi cha maswali na majibu kuisha, mwenyekiti huyo aliwatambua wafanyabiashara wengine waliotoa msaada kwa waathirika hao lakini hakugusia msaada ulitolewa na Mbowe.
Tuesday, September 13, 2016
Michuano ya hatua ya makundi ya michuano ya mabingwa barani ulaya imeanza hukutukishuhudia Barcelona ikiwaadhibu Celtic kwa kipigo kikali cha magoli 7 kwa sifuri
Matokeo mengine ni pamoja na PSg waliotoka sare ya magoli ya moja-moja na Arsenal.Kwingineko vijana wa Diego simeon wamepata ushindi ugenini mjini amsterdam dhidi ya PSV
Michuano hiyo ayaendelea tena siku ya leo kwa kikosi cha Real madrid,Manchester city,leicester city, kushika dimbani kunako hatua ya makundi
Monday, September 12, 2016
UEFA CHAMPIONS LEAGUE
UEFA champions league group stage
Barcelona vs celtic
Psg vs arsenal
Psv vs Atm
Mitanange yote saa 3:45
Barcelona vs celtic
Psg vs arsenal
Psv vs Atm
Mitanange yote saa 3:45
Subscribe to:
Comments (Atom)



